Makala
Mwanzo
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao

 

  MASWALI NA MAJIBU-Ndoa  


Ndoa na Talaka -Sehemu ya Tano                              
 
  1. Mimi nilikuwa Muislamu na nimeolewa na  mtu sio muislamu na sasa nimebadilisha dini, nimekuwa jewish. Je kuna tatizo mbele ya Mwe/M. Mimi ninachojua katika Uislamu haifai mwanamke kumbadilisha mwanaume kuingia katika dini nyingine. Kama upo uwezekano naomba uniambie.

  2. Jee, hali mke anaweza kumkatalia mumewe kukhusu maingiliano yao ya kijinsi,kwa sababu za mke kutaka kufanya ibada, kama kufunga,kusali suna au haja ya kusoma tasbeeh au  qur-aan,baada ya fardhi??

  3. mimi nilikuwa nina swali kwamba kama mtu ameoa baada ya hapo Mwenyezi Mungu akawajaalia mtoto sasa yule mwanaume anapaswa amuingilie mke wake baada ya muda gani hapo uislam unatuelezaje? na hapo hapo atakapomuingilia kuna dua gani inasomwa na jingine kwa kuongezea kwenye mada hii muislam unapomuingilia mke wako huwa kuna dua ambayo unasema ya Mwenyezi Mungu awajaalie kile kiumbe kitakachokuja kiwe miongoni mwa mja ambaye anatekeleza maamrisho ya Mwenyezi Mungu sasa basi kama huyo muislam anamuingilia mke pasina kutaka mtoto ni kwa ajili ya kukidhi haja zake  je hapo kuna dua gani inayosomwa? inshallah yangu ni hayo kama kuna mahala nimekosea naomba radhi binadamu ndio mkoseaji,

  4. Mimi ninabinti nataka kumuoa lakini kuna suala bado linanipa utata.
    1. Binti huyo alishaolewa miaka minne iliyopita huko nyumbani.
    2.Mara baada ya kuolewa alikaa siku chache kisha aliondoka kuja huku ulaya kwa masomo
    3. alikuwa akiwasiliana na mumewe kwa kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu.
    4.Baaada ya hapo akapata habari kwamba mumewe anafanya uzinifu na kazaa na mwanamke mwingine.
    5.cha kutatanisha zaidi mume huyo alikuwa mkristo kabla hawajaoana alibadili dini ili aweze kumuoa binti huyo.
    6.sasa hivi huyo bwana karudi kwenye ukristo na hakuna mawasiliano kati yao.
    SWALI NI HIVI NINAWEZA KUMUOA HUYU BINTI INGAWA HAJAPEWA TALAKA? AU NINI NIFANYE ILI NIWEZA KUMUOA BINTI HUYU.

  5. a-ni nani anayefaa kuozesha?
    b-je mtu ambaye hana mke na hajawahi kuoa anafaa kuozesha?

  6. MWANAMKE ALIKUWA AKIISHI NA MUMEWE NA WATOTO WAKE NA MDOGOWAKE WAKIKE, MARA YULE NDUGU AKASHIKA MIMBA ALIPO ULIZWA NA DADAAKE AKASEMA ALIYE NITIA MIMBA HII NI MUMEO YAANI SHEMEJIYAKEALIYE NDANI YA NYUMBA.AKAJIFUNGUWA NA MTOTO AKATOLEWA DAMU NI DAMU YA MUMEWE SAWA.AMEPATA USHAHIDI KAMILI.
     INAJUZU HUYU MWANAMKE KUENDELEA KUISHI NA MUMEWE KI MKE NA MUME?

  7. IKIWA MKE ANAISHI KATIKA NCHI ZA UARABUNI NA MUME ALIKWENDA AFRICA KWA AJILI YA MATIBABU, HUKO HUKO AKAFARIKI DUNIA.ILIPOKUJA KHABARI YA MUME AMEFARIKI, MKE AKATAKA KWENDA KUMZIKA MUMEWE PAMOJA NA WATOTO WAKE (MUHRIMU ZAKE) BAADHI YA MASHEKHE WAKAMWAMBIA HAIJUZU KUTOKA KWENYE NYUMBA YAKO, WENGINE WAKAMWAMBIA UNAWEZA UKATOKA LAKINI MAGHARIBI UWE UMEISHA FIKA,  NA WENGINE WAKAMWAMBIA UNAWEZA UKASAFIRI MADHALI NA WATOTO WAKO WAKIUME WOTE.
    SASA SUALA LANGU INAJUZU KUSAFIRI KWANI ALIKUWA ANAWAHI MAZIKO HUKO ANAKO KWENDA.

  8. NANI ATAKAYE WEZA KUTOWA IDHINI YA KUOLEWA KWA MTOTO ULIYE MLEA. 
    IKIWA MIMI NA MUMEWANGU TUMECHUKUWA WATOTO HOSPITAL TUKAWALEA MPAKA UMRI WA KUPEWA WAUME, IMETOKEA RISKI YA WACHUMBA KUJA KUWAPOSA SASA WATOTO HAWA ITATUJUUZIA SISI WALEZI KUTOWA IDHIN YA KUOLEWA AU ITABIDI IDHIN ITOKE MAHAKAMANI?

  9. suali langu ni ikiwa mwanamke anataka aachwe na mumewe kwa sababu ya kuto enjoy na huyo mume na hawezi kumwambia kama amuache,wakati huyo mume hana tatizo lolote, tatizo ni huyo m/ke ndio anajilazimisha tu kuishi na huyo mumewe,sasa kama kuna DUA yoyote ya kumuomba Allah ili iwezekane KUACHWA basi tunaomba tufahamishwe,kwani huyo m/ke anaona pia anapata dhambi kwani hana hamu hata ya kukaa na  mumuwe,na  anaona dhiki ktk maisha yake kwa kuishi tu na mtu ambaye hana mapenzi naye, na wala hamvutii,ni anaishi tu  kama hana budi na anampenda kama kawaida tu sio kama mke inavyotakiwa kumpenda mume.basi tunaomba msaada

  10. Suala langu ni kuhusu kurithi kwa watoto mali ya mama yao aliyefikwa na mauti. Je iwapo kuna mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa na ana ndugu waliozaliwa ndani ya ndoa, watagawana vipi mali ilyoachwa na mama yao? Kwa mfano iwapo watoto ni watatu na wote wa kiume. mmoja wa hao ni mtoto wa nje ya ndoa.  Je watagawana kama ilivyo kawaida ya urithi wowote au huyu mwana nje kwa kuwa hana haki kwa baba atapata zaidi


 

JIBU

 

Rudi Nyuma                                                  Endelea Mbele


| Tuandikie |