Makala
Mwanzo
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao

 

  MASWALI NA MAJIBU-Masuala mengine ya Dini  


Masuala mengine ya Dini -Sehemu ya Pili                              
 
  1. Maswali yangu leo nayajenga kutoka katika Qur'ani 5:5,9:28, na 9:95.
    Kwa muktasari Allah katika surat(Al-Maida 5:5) anasema:
    --Na chakula cha walio pewa Kitabu ni halali kwenu,
    --na chakula chenu ni halali kwao. .......)
    Pia Katika surat (Tawba 9:28/95) anasema:
    Katika Aya 28.Enyi mlio amini! Hakika washirikina ni najsi, .......)
    na Katika Aya 95. ......Hakika hao ni najsi, na makaazi yao ni
    Jahannamu,........)

    MASWALI:
    (1).Je, Washirikina hao kwa sasa ni akina nani? kati ya (Mayahudi,Wakristo
    na wengine mf. Mabaniani).?

    (2).Ni daraja gani hadi mtu aitwe kuwa 'mshirikina'?, ikiwa Ushirikina ni
    kuabudu kitu chochote kinyume na Mwenyenyezi-Mungu kama vile kuabudu
    (sanamu, ng'ombe, mtu, na Mitume wa Allah n.k): Sasa Je, anayemuabudu
    mtu/Mtume (yaani Mayahudi/Wakristo) kumfanya ni mungu, na anayeabudu sanamu
    au ng'ombe kumfanya ni mungu; Ni nani mshirikina haswa kati ya makundi haya
    mawili????.

    (3).Je, watu wakitabu hao ambao tule kwao kwa sasa ni wapi? na ibada zao
    wanazifanyia wapi? na wao wanaitikadi gani ya kuhusu Allah ni Mmoja?.

    (4).Je, ni aina gani ya chakula ambacho ni kharamu kula kwa washirikina (au
    hata soda, biskuti, embe nk.)? Maana huku maofisini ni mtihani, wananunuaga
    vitu kama soda, chips n.k halafu kisha twakaribishana sasa je, vipi
    hapo!!!!? (Ambao ni Mabaniani wanao abudu ng'ombe).

    (5).Je, kwakuwa wao ni najisi, itakuwaje baada ya kuchuwa Udhu wako barabara
    kisha ukagusana naye udhu wako utatenguka? Au Je, akigusa chakula
    ulichopanga kukila kitanajisika?

    (6).Akikupa zawadi kama Fedha, Nguo, Redio n.k usichuwe?

 

  1. Baada ya kufa Mtume muhammad kulikua na makhalifa wanne ambao wakiongoza dini hii ya kiislamu yaani Othmani, Abubakkar, aLY na Omar. Wakati wa uongozi wao waislamu walikuwa wakiwasikiliza, kuwaamini na kupanga mambo yao kua kitu kimoja. lakini baada ya kufa wao hivi sasa waislamu hatuna kiongozi hata mmoja anaetuunganisha katika dunia hii chini ya uislamu. Tunaamini kitabu cha allah kinatusaidia kutoungoza.
    Swali  Jee dini inatukataza kuwa na kiongozi wa kiislamu katika dunia hii ili tuwewamoja?
    Kitu gani kinatukwamisha sisi waislamu kuwa na kiongozi mmoja wa kislamu ili tuwashinde adui zetu chini ya ulimwengu huu? 

  2. suala langu ni nataka kujua mama yake mtume s.a.w alipokufa alikufa muislam au la pamoja na ami yake aliyemlea.

  3. tulisoma kwamba mwenyezimungu ana sifa ya kuongea kwa ushahidi kwamba aliongea na nabii Musa (a.s)..na maneno ya Allah hayana herufi wala sauti ..sasa basi naomba nifahamishwe vipi nabii Musa(a.s)alijua kama mola sasa anamtaka avue viatu ktk lile jangwa takatifu ....hali ya kuwa maneno yake mola hayana sauti wala herufi ?????

  4. Kutokana na Aya hiyo hapo chini ya (Surat Hajj 22:40): Allah Aliposema:
    . Wale ambao wametolewa majumbani mwao pasipo haki, ila kwa kuwa wanasema: Mola wetu Mlezi ni Mwenyezi Mungu! Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hawakingi watu kwa watu, basi hapana shaka zingeli vunjwa nyumba za wat'awa, na makanisa, na masinagogi, na misikiti, ambamo ndani yake jina la Mwenyezi Mungu linatajwa kwa wingi. Na bila ya shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anaye msaidia Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mtukufu. 
    ---------------
    (1)Je, ni watawa gani hao ambao wanaokusudiwa?, (inamaana ni masister na mapadre?). Na je, wanalitaja namna gani hilo jina la Allah?, (Au ndio zile nyimbo zao na matarumbeta)?
     
    (2)Je, Hayo masinagogi ni yapi?
     
    (3)Je, makanisani napo. WANALITAJA VIPI jina la ALLAH? (Au ni makanisa yapi hayo?)
    -------------
     
    Mimi nimeuliza maswali haya, hii yote nikutokana na mkristo mmoja, alinijia akanipa hii aya kisha akadai kwamba: Jina la Mwenyezi Mungu linatajwa kanisani halafu nyinyi mnasema ukristo sio dini vipi, mbona Muhammadi wenu anakudanganyeni?). Wallahi mimi nilishindwa jinsi gani nimjibu ili anielewe, nikakaa kimya. Na ndio mara yangu ya kwanza kuiona aya hii.
     
    Sasa nakuombeni munisaidie kwamba Allah aliposema hivyo ki-elimu amekusudia nini?, Watawa gani?, makanisa gani?, masinagogi gani?.

  5. SUALA LANGU NIKIOMBA KUULIZA IKIWA MTU AMEOKOTA PESA NJIANI  KATIKA MJI WA SAUDIA, AMEISHA MALIZA KUFANYA HIJA YAKE, ANARUDI KATIKA MJI WAKE. PAHALA HAPO HAPANA MAJUMBA KUNA PETROL STATION TU. JE ZINAMHALALIKIYA PESA ZILE KUZITUMIYA NAOMBA MNIFAFANULIYE. BI TAUFFIQ.

  6. Je! Inajuzu Kisharia Kulijengea Kaburi La Muislamu Kwa Saruji (Cement) Na Kuandika Jina Au Tarehe Au Hata Baadhi Ya Aya Za Quraan Juu Ya Kaburi Hilo? Ikiwa Jambo Hilo Halijuzu. Inajuzu Kubomoa Kaburi Baada Ya Kujengewa Kwa Saruji (Cement)? Tafadhali Naomba Ufafanuzi Na Jibu la yakini Ambalo Halina Shaka Katika Swala Hili muhimu.

  7. 1-  IKIWA MZAZI  YUHAI ALIWASIA  NIKIJA KUFA  MTOTO WANGU ASILIGUSE  JENEZA LANGU,KWA SABABU AMEOLEWA NA MUME MKIRISTO. JE INAMAANA YULE MTOTO AKIENDA KULIBUSU JENEZA LA MZEE WAKE. ITAKUWA NI HARAMU KWAKE.

  8. TUNAVYO JUWA KUMNYONYESHA MTOTO MAZIWA YA KIFUANI MTOTO ALIYEKUWA SI WAKO INAKUWA NA WATOTO WAKO WASHAKUWA NDUGU HAWAWEZI KUOWANA.
     JE MWANAMME AKATOWA DAMU  KUTIWA MTOTO WA KIKE ALIYE KUWA SI DADA YAKE INAMJUZIA KUMUOWA?

  9. swali langu ni kuku wanaochinjwa na wayahudi [jews] sisi waislam tunaruhusiwa kula?maana yake wengine wanasema wanafaa na wengine wanasema maadamu hakuna kalima iliyosemwa wakati wa kuchinja basi basi hawafai-tuondolee mushkeli sheikh kwa sababu sisi tunaishi ugenini huku

JIBU

 

Rudi Nyuma                                                  Endelea Mbele


| Tuandikie |