|
Ni suala lisilo
na shaka kwamba Uislamu umemfanya mtoto kuwa ni
haki ya shirika baina ya wazazi, baba na mama. Baba
kama mkuu wa familia ana sehemu ya haki na wajibu kwa mtoto kama
ambavyo mama mlezi wa familia pia ana haki na wajibu kwa mwanawe. Mtoto
katika Uislamu si wa baba pekee au wa mama pekee bali ni haki shirika
baina yao na pia jamii. Kwa hivyo ni jukumu la baba kuhakikisha kuwa
anampa mtoto katika utaratibu utaratibu ulionekana na sheria. Pia atambue
kwamba baada ya kumpata mtoto ana dhima kuu ya kumlea kwa maana ya malezi
kama atakiwanavyo na sheria. Ahakikishe anampa malezi ambayo yatamfanya awe ni tunu kwake yeye kama mzazi
(baba/mama) na kwa jamii yake.
Jamii
ifaidike nae na yeye afaidike nayo. Mtoto akiwa ni utaji/nembo ya mazazi
wake, pia haachi kuwa ni tofali linaloungana na matofali mengine katika
kuujenga ukuta imara (jamii). Ni suala lisilopingika kwamba uhai/uimara wa
jamii/umma unategemea kwa kiazi kikubwa nguvu kazi ya jamii/taifa hilo na
nguvu kazi hii kwa asilimia nyingi inategemea
ongezeko la watu na uwezo wao wa kufanya kazi.
Uislamu
umehimiza sana suala la uwekaji wa misingi imara ya nguzu kazi, heshima ya
mtu binafsi na umma/taifa, upanuzi wa makazi (mipango endelevu ya miji),
mgawanyiko wa madaraka na taifa kwa ujumla.
Misingi na malengo haya hayawezi kufikiwa kama khakuna ongezeko la watu
ambao litamaanisha ongezeko la nguvu kazi ya jamii/taifa husika. Uislamu
unaamini kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu amewaumba wanadamu na kuwaleta
ulimwenguni wazaane na kuijaza ulimwengu
sambamba na kuustawisha. Kwa mantiki hiyo Qur-ani tukufu imeraghibisha na
hadithi zimehimiza sana suala la ndoa pamoja na ukweli kwamba ndoa
ni suala la kiamumbile lisiloepukika. Hebu tuitupie jicho na fikra
za kuangalia neema ya Allah aya hii: ‘NA ALLAH AMEKUUMBENI WAKE KATIKA
JINSI YENU, NA AKAKUJAALIENI KUTOKA KWA WAKE ZENU WATOTO NA WAJUKUU. NA
AKAKURUZUKUNI VITU VIZURI VIZURI. BASI JE, WANAAMINI YASIYOKUWA YA HAKI
NA KUZIKATAA NEEMA ZA ALLAH? (16: 72)
Ukitaka kuijua
hadhi, daraja na nafasi ya watoto katika maisha haya, isome kwa mazingatio
kauli hi ya Mola Wako:” MALI NA WATOTO NI PAMBO LA MAISHA YA
DUNIA………” (18: 46)
Na huyu hapa
Mtume wako Rehema na Amani zimshukie akilizungumzia suala la ndoa na
kuzaana, hebu tumsikilize na tumuelewe :“Oaneni, mzaane, mtaongezeka,
kwani hakika mimi nitajifakharisha nanyi kwa nyumati zingine siku ya
Qiyama.
Kuna
mazingatio/sababu kuu mbili za msingi ambazo zinapeleka kuwepo na ulazima
wa jamii ya wanadamu kuoana na kuzaana kwa msingi ya sheria.
1.
Sababu ya kwanza ni ile haki ya jamii kwa mtoto kutokana na mchango
wake katika kuiendeleza jamii kama mwanajamii. Hili linatokana na ukweli
kwamba “ Mjenga nchi ni mwananchi, kwa hivyo ni dhahiri kwamba
jamii/taifa lolote haliwezi kupiga hatua yoyote ya kimaendeleo ila kwa
mchango wa nguvu kazi za wanajamii/wananchi wenyewe na khasa vijana ikiwa
sote tunakubaliana hivi, basi hatutashindwa kuiona flasafa ya Uislamu
katika kuhimiza suala la ndoa, na kuzaana.
2.
Sababu ya pili ni kutopingana na utaratibu wa maumbile aliotupangia
na kutuimbia Mola wetu kwa kuvizuia viungo vyetu kutekeleza jukumu/kazi
vilivyoumbwa kwa ajili hiyo tu. Sisi kama viumbe hatumiliki maumbile yetu na utendaji kazi wake na
hivyo basi hatuna haki ya kuuzuia au kuubadilisha utendaji kazi wake.
Kwani kufanya hivyo hakutamaanisha kingine zaidi ya kupingana na maumbile
ya Allah:…..”MOLA WETU NI YULE ALIYEKUPA KILA KITU UMBO LAKE KISHA
AKAKIONGOZA (kufuata kinachowafiki umbo lake hilo).” (20: 50)
“………..AMEUMBA
KILA KITU NA AKAKIKADIRIA KIPIMO (chake)” (25: 2)
“
ALIYEUMBA (kila kitu na) AKAKITENGENEZA. NA AKAKIKADIRIA (kila kimoja
jambo lake) NA AKAKIONGOZA (kufanya jambo hilo)” (87: 2-3).
UISLAMU
HAURIDHI WINGI USIOKUWA NA NGUVU.
Yanapokutana
pamoja mazingatio/sababu kwa mbili hizi tulizozitaja ambazo ni:
1.
Haki ya umma (jamii) na
2.
Haki ya maumbile
Zinazokutana
katika dharura/umuhimu wa kupatikana kizazi pia huungana pamoja tena
katika janibu (Upande) nyingine muhimu ambayo ni “uwajibu wa kuondoa
madhara”ambayo humfika mke au jamii. Madhara haya humsibu mama khasa
bali na jamii kwa ujumla kutokana na matumizi, mabaya ya uhuru wa kuoa na
kuzaa uliotolewa na Uislamu kama ambavyo maumbile yakiunga mkono na
sayansi ya tiba yasivyoukiri ujauzito wenye madhara kwa mama
au mtoto na kuwafikiwa na Uislamu, dini inayokubaliana na maumbile
ya mwanadamu:”……DINI ILIYO SAWA SAWA NDIO UMBILE ALLAH ALILOWAUMBIA
WATU (yaani dini hii ya
Kiislamu inawafikiana barabara na umbo la binadamu)…………”
(30:30.)
Kadhalika
ni kama hivyo, Uislamu hawakubali wala kuridhia wingi usiokuwa na
nguvukazi ya kuweza kujikimu wenyewe na kujilinda dhidi ya umma dhalimu.
Wingi huu hauwezi kumpa Mtume fursa ya kujifakharisha siku ya kiyama mbele
ya nyumati nyingine. Hivi ndivyo yanavyoashiria na kufahamisha maneneo
haya ya Bwnaa Mtume Rehema na Amani zimshukie:
“Mataifa yanakurubia kuitana pamoja dhidi yenu kama sisimizi
wanavyoitana kwenye sahani yao. Basi (hapo) akauliza mwenye kuuliza: Hivi
ni kutokana na uchache wetu wakati huo? (Mtume) akamjibu: Hapana, bali
nyinyi mtakuwa wengi, lakini wingi wenu huo utakuwa ni mithili lya
takataka zinazosombwa na maji na Allah ataondosha ataondosha utisho wenu
mioyoni mwa maadui zenu (mtakuwa hamtishi tena). Na atazionyesha nyoyo
zenu udhaifu. Akauliza muulizaji: Ni upi udhaifu huo, ewe Mtume wa Allah?
(Mtume) akajibu: Kuipenda dunia na kuchukia kufa: Abuu Daawoud.
Bila
ya shaka tukiielewa vema hadithi hi tutaona na kujua kwamba inaashiria
kuwa wingi usiokuwa na nguvu za kujihami uliotawaliwa na maradhi,
ukagubikwa na umasikini na kukumbatiwa na ujinga hauna kheri wala manufaa.
Jamii/uma uliosheheni
wajinga, masikini na wagonjwa, siku zote utakuwa ni uma ombaomba na
tegemezi. Hali hii ya kutegemea misaada itauodolea uma huuhaiba mbele ya
nyumati (mataifa) nyingine. Hautakuwa na sauti wala uhuru wa kujiamulia
mambo yake wenyewe bali ni sharti ufuate
mapenzi na matakwa ya bwana mtoa misaada. Uislamu sambamba na
kuhimiza watu kuzaana kwa lengo la kuisitawisha jamii ya wanadamu, pia
umesisitiza na kuulinda wingi
huo na udhaifu na kila lipelekealo udhaifu na kuufanya kama wingi wa
sisimizi unaoweza kusambaratishwa na kishindo kidogo tu. Uislamu ukaulinda
na kuuhifadhi wingi huu kwa kuweka vigezo/kinga zifuatazo:
a./
Kuhimiza afya njema ya mwili,
akili na itikadi dhidi ya maradhi mbalimbali. Hili linaweza kuonekana
kupitia mafundisho sahihi ya
Uislamu. Ndipo unaukuta Uislamu unampa ruhusa ya kula mchana wa mwezi wa
Ramadhani mgonjwa ili kumuepusha na kuzidiwa na maradhi. Unamtaka ale ili
kuiimarisha na kuijenga afya yake. Si hivyo tu bali umemruhusu hata
msafiri nae ale ili kuonyesha kuwa Uislamu unaithamini na kuipa umuhimu wa
kwanza afya yake na pia unatambua mashaka ya safari. Isitoshe
ukamuhalalisha mtu kutayamamu kwa kutumia udongo/mchanga badala ya kutumia
maji katika twahara ya udhu au josho, iwapo matumizi ya maji yatauzidisha
ugonjwa au kupelekea kuchelewa kupona au kupata kovu/dosari yoyote
mwilini.
Bila
ya shaka mtu mwenye kufuatilia kwa
makini vifungu vya sheria ya kiislamu atagundua kuwa
uzingatiaji wa siha njema (afya) na maradhi ndio msingi mkuu wa
hukumu nyingi kama sio zote. Zaidi ya yote hayo imekuja amri ya kuwataka
waislamu kufanya dawa na kujitibia katika kauli nyingi za Mtume wa Allah -
Rehema na Amani zimshukie. Bali yeye mwenyewe Bwana Mtume ameelekeza dawa
kadhaa za kutibu maradhi mbalimbali. Hii ni miongoni mwa kauli zake hizo
zenye kuitakia mema
jamii/umati wake: “Fanyeni dawa enyi waja wa MwenyeziMungu, kwani hakika
Mwenyezi Mungu Mtukufu hajaleta ugonjwa ila ameuwekea na dawa yake
isipokuwa ugonjwa mmoja tu Uzee”, Imam Ahmad.
Pia
ametahadhairhsa dhidi ya maradhi ya kuambukiza na hatua za kujikinga dhidi
ya maradhi hayo yanapoingia katika kitongoji/mji, akasema:
“Mtakapoisikia tauni iko mahala basi msitoke
kwa ajili ya kuikimbia (kwani kukimbia ni kuitoa hapo na kuieneza
huko mkimbiliako)” Bukhaariy
b./
Kumpa mmojawapo wa wanandoa haki ya kuvunja mkataba wa ndoa iwapo:
-
Itadhihirka
kwamba mmoja wao ana maradhi yanayojilikwamisha lengo la ndoa kutimia
-
Au
ana maradhi yanayoweza kumuambukiza mwenzi wake au kizazi chao.
Ikiwa
kama Uislamu unajifakharisha kwa wingi na unataka nguvukazi katika usitawi
wa jamii, basi unautaka uma/jamii uwe na wingi wenye nguvu, afya njema,
elimu na jhali bora ya kimaisha ili kulinda hadi, heshima na itikadi yao
sambamba na kuwa huru katika kuchagua.
|