Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao !!!

 

Nasaha za Dini  

"Dini ni nasaha, wakauliza kwa nani ? Akasema Mtume : Kwa Allah, Mtume wake, kwa viongozi wa waislamu na watu wa kawaida" Hadith Tukufu

UISLAMU NA SUALA LA FAMILIA-I

 

NDOA NA RIZIKI NJEMA...VI

Ndoa kama msingi mkuu wa familia si jambo jepesi ambalo huwa kwa, makubaliano na maridhiano baiana ya pande mbili, mwanamume na mwanamke ambao huamua kuchanganyika pamoja na kuanza maisha kama mtu na hawara yake. Hizi ni fikra potofu dhidi ya suala hili zito la ndoa, ni wajibu zisahihishwe. Ndoa ni suala lenye umuhimu wa pekee na nafasi kubwa katika Uislamu. Hili linatokana na kuwa kwake ndio msingi wa familia ambazo ndizo zinazounda jamii ya wanadamu. Ni kutokana na uzito wake huu ndio tunamkuta Mwenyezi Mungu Mtukufu analihusisha suala la ndoa na riziki njema, akasema, NA ALLAH AMEKUUMBENI WAKE KATIKA JINSI YENU, NA AKAKUJALIENI KUTOKA KWA WAKE ZENU WATOTO NA WAJUKUU NA  AKAKURUZUKUNI VITU VIZURI VIZURI…………”  (16:72)

Angalia jinsi Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyotuwekea utaratibu na mpango mzuri wa maisha yetu. Mpango huu si mwingine zaidi ya ndoa. Kupitia ndoa anaturuzuku bila ya maombi yoyote kutoka kwetu watoto, wajukuuu sambamba na riziki njema. Haya ni baadhi ya matunda peni ya utaratibu huu wa Allah kwetu sisi waja wake. Hakuna hata mmoja asiyeufahamu umuhimu wa watoto kwa wazazi, asiyejua umuhimu huu amuangalie mtu ambaye hajajaliwa kupata mtoto namna anavyohangaika huku na kule. Suala la riziki na umuhimu wake katika maisha yetu ya kila siku halina kificho kwa kila mmoja wetu. Ikiwa Mwenyezi Mungu Mtukufu anaithamini riziki njema kupitia ndoa, kipi basi kianchofanya uzini na ukaacha kuoa? Je, huiamini ahadi ya Mola wako, Mtoa riziki? NA WAOZENI WAJANE MIONGONI MWENU (waungwana) NA WALIO WEMA KATIKA WATUMWA WENU(wanaume) NA WAJAKAZI WENU, KAMA WATAKUWA MAFAKIRI ALLAH ATAWATAJIRISHA KATIKA FADHILA ZAKE, NA ALLAH NI MWENYE WASAA, MWENYE KUJUA: (24:32).

UIMARISHAUJI WA MAFUNGAMANO BAINA YA MUME NA MKE……VII

Uhusiano mwema masikilizano na maelewano ndani ya nyumba ni miongoni mwa mambo ambayo yanaimarisha mafungamano haya ya ndoa baina ya mume na mke. Kuwepo kwa mafungamano imara baina ya wawili hawa kupelekea kuzidi kwa mapenzi, huruma na utulivu. Nyumba iliyosheheni mapenzi, huruma na utulivu, huwa ni pumbazo la nafsi na raha yenye furaha kwa kila mmoja, mume na mke. Hili ndilo analolisema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kauli yake NA KATIKA ISHARA ZAKE (za kuonyesha ihsani zake juu yenu) NI KUWA AMEKUUMBIENI WAKE ZENU KATIKA JINSI YENU ILI MUPATE UTULIVU KWAO, NAYE AMEJAALIA MAPENZI NA HURUMA BAINA YENU……..” (30:21) Mwanadamu hawezi kuifurahia neema ya watoto wala hawai pambo a masiha yake kama nyumba yake haikutawaliwa na utulivu  na akaishi chini ya anaga la mapenzi na huruma na hapo ndipo mke na watoto huwa ni burudani ya macho aliyoileza Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kauli yake tukufu. (NA WALE WANAOSEMA: “ MOLA WETU! TUPE KATIKA WAKE ZETU NA WATOTO WETU YABURUDISHAYO MACHO( yetu) nyoyoi zetu) NA UTUJAALIE KUWA WAONGOZI KWA WAMCHAO (Allah) “  (25:74)

Ni kutokana na umuhimu huu wa suala la ndoa kwa mwanadamu ndio maana Uislamu ukaishughulikia sana ndoa. Uislamu ukaiwekea ndoa sheria na kanuni madhubuti zenye dhima ya kuhakikisha inafikia kilele cha malengo yake. Sheria na kanuni hizi zinamjengea mwanadamu mazingira bora, mazingira tayarifu ya ndoa. Miongoni mwa aya za Qur-ani Tukufu na hadhithi za Mtume zinatoa maelekezo juu ya ndoa ni hizi zifuatazo:

i)                   Uchaguzi wa mke/mume

Tunasoma kuhusiana na suala zima la uchaguzi wa mke:”……BASI WANAWAKE WEMA NI WALE WENYE (waume zao) KWA KUWA ALLAH AMEWAAMRISHA WAJIHIFADHI……” (4:34)

Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie – anatupa vigezo vya kuolewa mwanamke kupitia riwaya iliyopokelewa na Abu Hurayrah Allah amuwiye radhi – kutoka kwa Mtume amesema:

Mwanamke  huolewa kwa mambo manne:

  1. Kwa mali yake

  2. Na uzuri wake

  3. Na nasabu zake

  4. Na dini yake. 

Basi mchague mwenye dini itabariki mikono yako” Jaamiy swaghiyr. Ili kujenga familia bora Uislamu haukomelei tu kumpa mwanamume vigezo vya kuchagua mke mwema na kumsahau mwanamke kwa kuzingatia kuwa ni mwanamke na mwanamume pamoja ndio wanaounda ndoa, Uislamu umemuelekeza mwanamke pia amchague nani kuwa mume mwandani na mshiriki mwenza katika maisha. Kigezo pekee ni dini na tabia kama alivyoeleza Bwana Mtume-Rehema na Amani Zimshukie.

ii)                 Ahadi Thabit

Uislamu kwa kuizingatia dhima na umuhimu wa ndoa katika maisha ya mtu binafsi familia na jamii umeifanya ndoa kuwa ni mkataba. Mkataba huu unahusisha mambo yafuatayo kama nguzo.

1.    Matamko ya “Iijaab” na Qabuul”

Ø     “Ijabu” hili ni  tamko linalotoka wa walii wa mwanamke kumwambia muaoji (mume mtarajiwa) wakati wa kufunga mkataba huu. Tamko hili ni kusema “NIMEKUUOZA “ Fulani.

Ø     “Qabuul” hili ni tamko analolitamka muoaji kumwambia walii. Husema “NIMEKUBALI KUMUOA” Fulani

 

2.    Mashahidi.

Hawa ni watu watakaoshuhudia mkataba wa ndoa ukifungwa.

3.    Walii wa mke.

Huyu ni mtu mwenye mamlaka ya kumuozesha mwanamke. Huyu ndiye anayeusimamia mkataba huu kwa niaba ya mwanamke, kwa sababu katika Uislamu mwanamke hajiozeshi yeye mwenyewe. Mtu huyu huwa ni baba mzazi, baba mzaa baba, kaka wa tumbo moja, mwanawe kaka, ami (baba mdogo/mkubwa) na kuendelea kama walivyobainishwa katika vitabu vya fiq-hi.

4.    Bwana na Bibi harusi (mume na mke)

Hawa ndio wanopeana ahadi thabiti ya kuishi kama mume na mke chini ya muongozo na maelekezo ya Mola jwao. Hupeana ahadi ya kushirikiana katika matamu na machungu ya maisha. Hupeana ahadi ya uaminifu na ukweli ya kwamba kila mmoja wao atachunga heshima ya mwenziwe, hataisaliti ndoa yao. Ahadi hii wanayopeana katika mkataba huu haina budi kulindwa na kuheshimiwa na kila mmoja wao. Kwa sababu ndio inayowaunganisha pamoja kimwili, kiroho na kijinsia ikawafanya wakazoeana kwa muda mfupi tu kuliko hata ndugu waliozaliwa na baba na mama mmoja. Hii ndio ahadi thabiti ndani ya kitabu chako kitukufu. “NA KAMA MKITAKA KUBADILISHA MKE MAHALI PA MKE (yaani kumuoa mke mwingine na kumuacha huyo wa zamani) NA HALI MMOJA WAO (naye ndiye huyo unayemuacha) MMEMPA MRUNDI WA MALI, BASI MSICHUKUE CHOCHOTE (msimnyang’nye). JE, MNACHUKUA KWA DHULMA NA HATIA ILIYO WAZI? NA MTACHUKUAJE NAHALI NYINYI KWA NYINYI MMEINGILIANA? NAO (wanawake) WAMEPOKEA KWENU AHADI THABITI (kuwa  mtakaa nao kwa uzuri)” (4: 20-21)

Katika kuutekeleza mkataba huu wa ndoa na kumtekelezea mke haki yake, Mwenyezi Mungu Mtukufu anatuambia: ‘ NAO (wanawake) WANAYO HAKI KWA SHARIA (kufanyiwa na waume zao) KAMA ILE HAKI ILIYO JUU YAO KUWAFANYIA WAUME ZAO….” (2:228)

KUZAANA NI MAENDELEO YAKIMAUMBILE YA KIZAZI CHA WANADAMU…….VIII

Mwenyezi Mungu Mtukufu amemleta mwanadamu katika maisha haya kwa lengo maalum. Ili aweze kulitekeleza lengo hili akamuandalia na kumuwekea utaratibu maalum utakaomletea kaika uhai huu, mahala pa kulitekelezea lengo la uumbwaji wake. Kwa upande mwingine mwanadamu ameumbwa katika maumbile ya kupenda kuishi milele bila ya kufa. Lakini hili ni jambo asilolimiliki, kwa hiyo njia pekee ya kuishi milele na kuendelea kukumbukwa ni kupitia kuzaana katika ndoa. Akipata watoto ataitwa baba/mama , babu/bibi hata baada ya kufa kwake bado familia yake itaendelea kujifakharisha na kujiita kwa jina lake (kujinasibisha nae). Kwa hivyo basi ndoa inakuwa ni sababu aliyoiweka Allah ya kuendeleza kizazi cha wanadamu, tusome, NA ALLAH AMEKUUMBIENI WAKE KATIKA JINSI YENU NA AKAKUJAALIENI KUTOKA KWA WAKE ZENU WATOTO NA WAJUKUU NA AKAKURUZUKUNI VITU VIZURI VIZURI…….” (16:72)


 

 


Forum | Guestbook | Tuandikie |