|
Naam,
ni kweli kuwa Uislamu umempa ruhusa mwanamke atoke nyumbani kwake kwenda
kufanya kazi. Lakini ni vema tukakiri kuwa hakuna ruhusa/uhuru usio na
mipaka, je, aende kufanya kazi katika mazingira gani? Tufuatane pamoja,
hatua kwa hatua:-
1.
Apewe idhini na mumewe au walii wake, yaani babu, baba, kaka, ami
na kadhalika. Tumeona katika somo lililopita kwamba wanawake wanatakiwa
wawaombe waume zao idhini/ruhusa ya kwenda msikitini kwa mujibu wa hadithi
ya Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie. Sasa iwapo kwenda msikitini
kunahitaji idhini ya mume, basi ni aula (bora) zaidi kutoka kwenda kufanya
kazi kupate idhini na baraka zote za mume. Bwana Mtume – Rehema na Amani
zimshukie – anasema katika kubainisha haki za mume kwa mkewe:
“…….Na wala (mwanamke) asitoke nyumbani kwake ila kwa idhini yake
(mume). Ikiwa atafanya hivyo (atatoka bila ya ruhusa ya mumewe) watamlaani
malaika wa mbingu na malaika wa adhabu mpaka atakaporejea (nyumbani kwake)
Twabaraany.
2.
Aende kazini na afanye kazi il-hali akiwa amevaa mavazi ya heshima
na sitara kama sheria inavyomtaka. Nguo zisiwe.
-
Nyepesi
zinazoonesha rangi ya mwili.
-
Zenye kubana
kiasi cha kuliacha finyango la mwili kuonekana na aonaye.
-
Na mapambo ya
kuvutia mno kiasi cha kuwashawishi wanamume kumkazia macho.
3.
Asikae faraghani, peke yake na mtu ambae si maharimu yake hata kama
ndie bosi wake kazini. Lazima awe katika mazingira ya watu wengine ambapo
farahga mazingira ya watu wengine ambapo faragha haina nafasi.
4.
Usiwepo msongamano utakaopeleka kugusana wanamume na wanawake kama
inavyokuwa masokoni, katika vyombo vya usafiri na kadhalika.
5.
Kazini kuwepo na mazingira ya amani ambayo yatamdhamini kutokufikwa
na matendo yote mabaya, ya fedheha na yenye kuudhalilisha utu wake. Kama
vile kufanya kazi mahala pa uchafu, katika vilabu vya pombe, nyumba za
kulala wageni, mahoteli ya kitalu, mahala panapochezwa kamari, humu mote
ni mahala ambapo mwanamke anaweza kudhalilishwa kijinsia kwa kubakwa au
kudhalilishwa kisaikolojia kwa kutukanwa na mambo mengine machafu yenye
kufanana na hayo.
6.
Kazi isimzuie kutekeleza wajibu wake kwa Mola wake, mumewe na
wananwe, kwani kutokutekeleza wajibu ni haramu. Kwa mantiki
hiyo kila linalopelekea kutokutekeleza wajibu nalo litakuwa ni
haramu.
Haya
ndiyo mazingira ambamo mwanamke wa Kiislamu anaruhusiwa kufanya kazi .
Naam
ni ukweli, ndiyo ni ukweli uliodhahiri na usiopingika kwamba kila uma
duniani una nembo yake rasmi ambayo inautambulisha uma huo mbele ya
nyumati nyingine, nambo hiyo
huundwa na mila, desturi na utamaduni wao. Vyote hivi huonekana kupitia
namna yao ya kula, kunywa, mavazi maskani na sanaa zao mbalimbali. Mambo
yote haya ndio huonesha na kutoa picha ya ustaarabu na itikadi za uma
husika.
Mwenyezi
Mungu Mtukufu amewaumba watu wakiwa wanatofautiana katika mambo mengi, na
tofauti hii itaendelea kuwepo mpaka mwisho wa dunia. Ukweli huu usio na
shaka unajidhihirisha kupitia kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: “ NA KAMA
MOLA WAKO ANGALIPENDA, ANGALIWAFANYA WATU WOTE KUWA UMATI MMOJA. (
Angaliwafanya wote kufuata kitu kimoja. Lakini amewapa akili na nguvu ya
kutumia akili zao hizo watakavyo, ikiwa kwa wema au ubaya.)
KWA HIVYO WATAENDELEA TU KUHITILAFIANA. ISIPOKUWA WALE AMBAO MOLA
WAKO AMEWAREHEMU. NA KWA (rehema) HIYO MUNGU AMEWAUMBA (ila wenyewe tu hao
wengine wamekhitari mabaya) NA LITATIMIA NENO LA MOLA WAKO (la kuwa):
KWELI KWELI NITAIJAZA JAHANAMU KWA MAJINI A BINADAMU WOTE (walio wabaya).
(11:118-119).
Uzuri
au ubaya wa utamaduni wa jamii Fulani ya watu unategemea kwa kiasi kikubwa
mtizamo wa jamii nyingine ya nje. Ni wazi kuwa utamaduni unaoonekana mzuri
tu kwa jamii Fulani ukawa ni mbaya machoni mwa jamii nyingine. Mwanamke wa
kihindi mathalan ana vazi lake rasmi lijulikanalo kama “Saari” vazi
hili ndilo humtambulisha mbele ya jamii nyingine kuwa yeye ni nani.
Mwanamke huyu hulionea fakhri vazi lake hili na hulivaa popote pale
ulimwenguni hata kama anashiriki katika vikao vikuu vya jumuia za
kimataifa. Kwa kuwa ni utamaduni wake, yeye binafsi haoni haya kulivaa
vazi lake hilo na hakuna yeyote aliyethubutu kumkosoa au kumlaumu kwa
uvaaji wake huo, hata, wale watu wa nchi za magharibi wanaojidai kuwa ni
mabingwa wa kukosoa na mahodari wa kusema. Pengine linaweza likawa si vazi
la kikazi, lakini ndio vazi linalovaliwa na mwanamke muhindi mlalahoi na
hata aliyekuwa Waziri Mkuu bibi Indra Ghandi. Bado hakuna aliyethubutu
kusema kuwa vazi hili la “Saari” linamzuia mwanamke huyu wa kihindi
kufanya kazi mbalimbali za uzalishaji.
Mwanamke
wa Ulaya mpaka mwanzoni mwa karne ya ushirini (20thC) alikuwa
akifunika kichwa chake na kuvaa mavazi marefu na hakukuwepo na wa kumlaumu
au kumkosoa. Lakini taratibu kwa kigezo cha kile kinachodaiwa maendeleo na
kwenda na wakati akaanza kulibadili vazi lake hili mpaka kufikia hapa
lilipo leo, likimuacha bila ya sitara na kuifanya bishara ya Mtume-Rehema
na Amani zimshukie “itimie”
Makundi mawili ya watu wa motoni sijayaona (bado katika uhai wangu) watu
wenye fimbo kama mikia ya ng’ombe wanawapiga watu, na wanawake waliovaa
na il-hali wako uchi, watembeao kwa maringo……………………”
Muslim.
Ama
mwanamke muislamu anayemuamini Allah, Mtume wake na
siku ya kiyama, Uislamu unamtaka avae mavazi ya sitara. Mavazi
ambayo kumsababishia usumbufu na uchokozi kutoka kwa wanaume na natija yake ikawa
ni kudhalilishwa kijinsia. Na si sahihi kusema kuwa vazi hili la kiislamu
linamnyima uhuru mwanamke kushiriki vema katika kazi mbalimbali za
kimaendeleo. Kwani tumewashuhudia wanawake wengi katika nchi zenye
Waislamu wengi wakifanya kazi katika taasisi na mashirika mbalimbali ya
kibinafsi na hata yale ya kiserikali, yakiwemo mashirika ya ndege
wakifanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa kabisa. Mavazi yao hayakuwa na wala
hayajawa na kikwazo katika utendaji wao wa kazi na majukumu yao kama
sehemu muhimu ya jamii. Kwa hivyo tuhuma hizi hazina msingi wala hoja
itokanayo na utafiti wa kielimu. Hizi ni kelele za watu wa magharibi
wanaotaka kuona mila, desturi na utamaduni wao unaitawala dunia na hili ni
kinyume kabisa na maumbile waliyoumbiwa wanadamu.
Kutokana
na wepesi wa dini hii inayokubaliana na maumbile ya mwanadamu, imemruhusu
mwanamke kutoka kwenda kufanya kazi na wala haikumfungia ndani tu kama
inavyodaiwa. Kulichofanywa na dini hii ni kumuandalia mazingira bora
ambamo humo ataweza kufanya kazi kwa amani na utulivu bila ya kudhallishwa
wla kubughudhiwa na yeyote awaye. Ikamjengea ukuta wa kumkinga na madhara,
kero na maudhi yanayoweza kumpata kutoka kwa wanajamii wengine. Ni wajibu
wake na yeye pia ajizuie kuwaudhi au kuwasababishia wengine kero/madhara
kwani mwanamke, mwenyewe ndiye chanzo cha madhara mengi yanayomsibu hivi
sasa. Lau angelishikamana barabara na dini yake na akatambua kwamba Hijabu
ni haki yake na ipo kwa maslahi yake asingefikia hapa alipo leo ambapo
anaonekana kama ni chombo cha kutangazia matangazo ya biashara na
kumstarehesha mwanaume, akinunuliwa kama bidhaa dukani/sokoni. Angelibakia
na utu na heshima yake kama mwanamke na mama wa jamii.
Mtu
anaweza kuthubutu kusema kuwa, baadhi ya kazi zinahitaji vazi rasmi.
Tunasema kuwa kazi haiwezi kuwa ni sababu/ruhusa ya kuvunja sheria ya
Mwenyezi Mungu Mtukufu, ambae ndiye aliyemuamrisha mwanamke kuvaa vazi la
sitara. Aliyeweka sheria ya kuvaa vazi fulani mahala fulani ni jamii,
swali ni je, tuitii sheria ya Allah isiyo na upungufu au utitii kanuni
iliyowekwa na mwanadamu mpungufu? Tusome: “KISHA TUMEKUWEKA JUU YA
SHARIA YA AMRI YETU, BASI IFUATE, WALA USIFUATE MATAMANIO YA WALE WASIOJUA
(kitu) KWA YAKINI HAO HAWATAKUFAA CHOCHOTE
MBELE YA ALLAH…………..” ( 45:18-19]
|